Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Stephane Aziz Ki ndiye Mfungaji Bora kwenye NBC Premier League msimu huu wa 2023/24 akiwa na jumla ya magoli 21.
Aziz Ki amefunga mabao matatu (hat-trick) kati ya mabao manne ambayo Yanga wameshinda kwenye ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Tanzania Prisons katika Dimba la Azam Complex, Chamazi.
Aziz Ki amefikisha magoli 21 kwenye Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara mpaka mechi ya mwisho ya msimu huu huku aliyekuwa akifukuzana naye, Feisal Salum Abdallah akifunga bao moja dhidi ya geita kwenye ushindi wa mabao 2-0 na kufikisha mabao 19.
Kabla ya hapo nyota hao walikuwa wakilingana baada ya kila mmoja kufunga mabao 18.
Aziz amekuwa na msimu bora sana, na hii ni hat-trick ya pili kwa Aziz Ki msimu huu ambapo hat-trick ya kwanza alifunga dhidi ya Azam Fc kwenye mzunguko wa kwanza katika mechia ambayo Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 3-2.
FT: Yanga 4-1 TZ Prisons (Aziz Ki 11’, 12’, 79’, Musonda 52’ / Ngasa 4’)
Full Time|
Simba 2-0 JKT Tanzania
Yanga SC 4-1 Tz Prisons
Geita Gold 0-2 Azam FC
Singida FG 2-3 Kagera
Mashujaa 3-0 Dodoma
Namungo 3-1 Tabora Utd
Coastal Union 0-0 KMC
Ihefu 5-1 Mtibwa Sugar.
#NBCPL: Goli la kwanza la Yanga limewekwa nyavuni na Aziz Ki
— Azam TV (@azamtvtz) May 28, 2024
Yanga 2-1 TZ Prisons (Aziz Ki 11’, 12’ / Ngasa 4’)
LIVE #AzamSports3HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #SokaLetuBambam #SokaLetuDamdam #MechiNaneLIVE #MechiZoteLIVE #AzamTV #EndOfSeason pic.twitter.com/IVcjve11Qo
#NBCPL: Chuma ya 20 kwa Stephane Aziz Ki
Yanga 2-1 TZ Prisons (Aziz Ki 11’, 12’ / Ngasa 4’)LIVE #AzamSports3HD
— Azam TV (@azamtvtz) May 28, 2024
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #SokaLetuBambam #SokaLetuDamdam #MechiNaneLIVE #MechiZoteLIVE #AzamTV #EndOfSeason pic.twitter.com/xu4eV4HtDS
#NBCPL: Chuma ya tatu kwa Yanga ikiwekwa nyavuni na Kennedy Musonda.
— Azam TV (@azamtvtz) May 28, 2024
Yanga 3-1 TZ Prisons (Aziz Ki 11’, 12’, Musonda 52’ / Ngasa 4’)
LIVE #AzamSports3HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #SokaLetuBambam #SokaLetuDamdam #MechiNaneLIVE #MechiZoteLIVE #AzamTV… pic.twitter.com/4bhuYShI7d
#NBCPL: Goli la 21 kwa Aziz Ki na ni hat trick yake ya pili msimu huu.
FT: Yanga 4-1 TZ Prisons (Aziz Ki 11’, 12’, 79’, Musonda 52’ / Ngasa 4’)
— Azam TV (@azamtvtz) May 28, 2024
LIVE #AzamSports3HD
#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #SokaLetuBambam #SokaLetuDamdam #MechiNaneLIVE… pic.twitter.com/PWKoO0sd7T