Thu, 14 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klqbu ya Azam imeingia mkataba wa miaka miwili na kiungo mshambuliaji, Mghana James Akaminko, akitokea Great Olympic.
Akaminko, 26, ambaye ni mmoja wa viungo wabunifu, aliwahi kucheza soka la kulipwa nchini Tunisia katika timu ya US Tataouine, pia amepita kwa vigogo wa Ghana, Ashanti Gold na Medeama.
Mbali na kucheza eneo la ushambuliaji, pia anao uwezo wa kucheza kama kiungo mkabaji, na anakuja kuongeza nguvu katika eneo la kiungo kuelekea msimu ujao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live