Thu, 6 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mazungumzo kati ya Vipers SC na mshambuliaji wao Yunus Sentamu ya kuongeza mkataba wake kusalia kunako klabu hiyo yamesimama.
Mshambuliaji huyo anataka kuondoka kunako klabu hiyo baada ya miaka 4 na klabu hiyo.
Klabu kutoka India wapo katika mazungumzo na wawakilishi wa mchezaji huku pia AZAM kutoka Tanzania nao wapo kwenye mazungumzo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live