Klabu ya Azam FC imetangaza kauli mbiu ya "La Revancha!" ikiwa na maana ya "Kisasi" kuelekea mchezo wake wa marudiano Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya Bahir Dar Kenema FC ya Ethiopia siku ya Ijumaa saa 1:00 usiku.
Klabu ya Azam FC imetangaza kauli mbiu ya "La Revancha!" ikiwa na maana ya "Kisasi" kuelekea mchezo wake wa marudiano Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya Bahir Dar Kenema FC ya Ethiopia siku ya Ijumaa saa 1:00 usiku. Mchezo wa kwanza ambao Bahir walichezea nyumbani kwao Ethiopia, waliibuka na ushindi goli 2-1 hivyo Azam wanao mlima wa kupanda ili kupindua matokeo hayo waweze kusonga hatua inayofuata.