Mwamuzi Omary Mdoe aliyekuwa akichezesha mchezo kati Azam FC dhidi ya Kitayosce ameamua kumaliza mchezo kabla ya muda baada ya Wachezaji wawili wa Kitayosce akiwemo Golikipa kuumia, hivyo kufanya Kitayosce kubakiwa na wachezaji 6 tu uwanjani.
Awali Tabora United iliingiza wachezaji nane tu uwanjani ambao ndio waliokidhi vigezo vya kucheza mchezo huo. Mchezo ukiwa unaendelea wachezaji wao 2 waliumia hivyo wakasalia 6 hali iliyopelekea mchezo kushindwa kuendelea kwa mujibu wa kanuni ya 17 (31) ya Ligi Kuu timu ikiwa na wachezaji pungufu ya 7 mchezo hauwezi kuendelea
Hadi dakika ya 12 Azam walikuwa wanaongoza bao 4 kwa 0, mabao matatu yaliyofungwa na Feisal Salum huku moja likifungwa na Prince Dube.
Mpaka mchezo huo unamalizika, Azam FC 4-0 Tabora United.