Mon, 8 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Azam FC wamefuata nyanyo za Yanga SC kwa kufurushwa kwenye mashindano ya Mapinduzi Cup.
Azam ambao ndio walikuwa wa kwanza kucheka na nyavu katika mchezo huo uliopigwa jioni hii katika Uwanja wa Amaan visiwani Zanzibar, walijikuta wanapoteza mchezo baada ya Singida kusawazisha na kuongeza goli katika kipindi cha pili.
Singida wanaungana na APR kufuzu hatua ya Nusu Fainali na sasa anasubiriwa Simba SC usiku wa leo kujua hatma yao watakapovaana na Jamhuri katika mchezo mwingine wa Robo Fainali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live