Thu, 5 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Azam FC, Yannick Bangala, amechanika msuli wa nyuma ya paja, kwenye mchezo wao wa juzi Jumanne dhidi ya Dodoma Jiji.
Baada ya mechi hiyo, Bangala alirudi Dar Es Salaam kwa vipimo zaidi, wakati timu ikielekea Tanga kwa ajili ya mchezo dhidi ya Coastal Union, Oktoba 6.
Baada ya vipimo ndiyo itajulikana ukubwa wa tatizo na muda wa matibabu hadi kupona.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live