Thu, 30 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Azam FC wameitandika timu ya kukusanya mapato ya KMC bao 2-1 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye uwanja wa Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Mabao ya Azam yamefungwa na mshambuliaji wake, Mkongo Idris Mbombo dakika ya 35 na Mzimbabwe Prince Dube dakika ya 71 wakati la KMC limefungwa na Matheo Anthony dakika ya 77.
Azam wamekuwa wakitumia nafasi ya mapumziko kuendelea kujenga timu yao kuelekea mashindano ya NBC League na kombe la Shirikisho la ASFC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live