Sun, 12 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bado jinamizi la mfuendelezo wa matokeo ya ushindi linaendelea kuitafuna Azam FC, baada ya hii leo kulazimishwa sare ya bila kufungana na Kagera Sugar ndani ya dimba la Azam Complex Chamazi.
Mchezo huo wa raundi ya nane Ligi Kuu Bara, ulimshuhudia mshambuliaji hatari wa Azam ambae alikosekana uwanjani kwa kipindi kirefu kutokana na kufanyiwa upasuaji, Prince Dube.
Mpaka dakika 90 zinakamilika, hakuna timu iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake na hivyo kugawana pointi.
Matokeo hayo yanatoa ishara mbaya kwa mwalimu George Lwandamina ambae miezi kadhaa aliongezewa Mkataba klabuni hapo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live