Mon, 6 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Azam FC, Awesu Awesu amejiunga na Klabu ya KMC kwa mkopo wa mwaka mmoja tayari kuwatumikia watoza ushuru wa Manispaa ya Kinondoni kwa msimu mzima.
Hivi karibuni Awesu Awesu alionekana katika Mashindano ya Ndondo Cup, akiitumikia timu ya Tabata All Stars.
Changamoto ya namba ndani ya kikosi cha Azam FC, imekua kubwa hivyo kiungo huyo kutafuta eneo ambalo atapata nafasi.
Awesu ametambulishwa leo Septemba 6, kitu kinachothibitisha kuwa alishasajiliwa kwani Dirisha la Usajili limeshafungwa tangu Agosti 31.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live