Thu, 8 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Zamalek ya Misri imetangaza kusitisha mkataba wa mchezaji Zakaria Al-Wardi, baada ya mchezaji huyo kuwaambia viongozi wa klabu hiyo kuwa anasumbuliwa na msongo wa mawazo, hali inayomfanya ashindwe kusalia klabuni hapo.
Kiungo huyo wa zamani wa Raja Casablanca mwenye umri wa miaka 24 alijiunga na Zamalek mwezi Agosti mwaka huu
"Tunamshukuru Zakaria Al-Wardi kwa muda aliokaa nasi, atarudisha pesa alizochukua na kukatisha mkataba kwa makubaliano" sehemu ya taarifa ya Zamalek.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live