Fri, 8 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo mkabaji wa Yanga, Khalid Aucho amefanyiwa upasuaji mdogo wa goti ambao utamuweka nje ya uwanja kwa muda kidogo.
Kutoka na upasuaji huo, Aucho anatarajiwa kurudi uwanjani baada ya wiki tatu kuanzia sasa, hivyo atakosekana kwenye michezo kadhaa.
Aucho mara ya mwisho kuitumikia Young Africans SC kabla ya kufanyiwa upasuaji huo ilikuwa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika Kundi D ugenini dhidi ya Al Ahly, Machi 1, 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live