Mon, 17 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo mpya mshambuliaji wa Simba SC, Aubin Kramo Kouame, anatarajia kujiunga na kambi nchini Uturuki leo Julai 17, 2023 mchana.
Kwa mujibu wa Simba APP, kiungo huyo anatarajia kujiunga leo mara baada ya kuanza safari jana akitokea nchini kwao Ivory Coast.
Nyota wengine wa tatu wa Simba, Che Malone, Jean Baleke na Willy Onana, wameondoka leo kuelekea nchini Uturuki kuungana na kundi la kwanza la wachezaji waliotangulia kuweka kambi wiki iliyopita.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live