Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aston Villa wanataka kumsajili Philippe Coutinho

Philippe Coutinho.jpeg Phillipe Coutinho

Tue, 10 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Aston Villa wanataka kumsajili Philippe Coutinho. Hii ni kwa mujibu wa Fabrizio Romano, ambaye anaripoti kwamba uhamisho wa Mbrazil huyo utajadiliwa msimu huu wa joto na Barcelona.

Kocha wa Villa, Steven Gerrard amebainisha kuwa anataka klabu hiyo imsajili Coutinho pale mkopo wake utakapokamilika mwishoni mwa msimu. Coutinho alijiunga na Villa wakati wa uhamisho wa Januari.

Coutinho, aliyezaliwa na kukulia huko Rio de Janeiro, alijiunga na Barcelona kutoka Liverpool – ambapo alicheza pamoja na Gerrard – kwa kitita cha €135m mwaka 2018.

Lakini alishindwa kufanya vyema Camp Nou na kukamilishauhamisho wa kopo kwa mkopo Bayern Munich kwa msimu wa 2019/20.

Inaonekana siku zake za kukaa Catalonia zimehesabika na mpango wa kurejea Uingereza ukiwa karibu mno. Coutinho amefunga mabao manne na asisti tatu katika mechi 15 alizoichezea Villa hadi sasa msimu huu.

Coutinho anahitaji kucheza mara kwa mara ili kumsaidia kupata nafasi katika kikosi cha Tite cha Brazil kwa ajili ya Kombe la Dunia nchini Qatar.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live