Klabu ya Al Ahly imesitisha usajili wa golikipa wa klabu ya National Bank ya Misri Mohamed Abou Gabal "Gabaski" siku tatu baada ya kumsajili kwa mkopo kuziba nafasi ya El Shanawy aliyeumia akiitumikia timu ya Taifa ya Misri.
Chanzo cha kusitishwa kwa mkataba huo ni kutokana na kutokuelewana kati ya nyota huyo na mshambuliaji wa klabu ya Al Ahly Mahmoud Kahraba wakiwa kambini nchini Misri.
Jambo hilo lilipelekea pia kutokuwa na maelewano mazuri kati yake na nyota wengi wa Al Ahly waliokuwa kwenye kambi ya timu ya Taifa kitu ambacho kimeilazimu Al Ahly kusitisha mkataba wake ili kuepuka mpasuko kwenye kikosi hicho.