Sun, 24 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Meneja wa Arsenal, Mikel Arteta amesema mshambuliaji Eddie Nketiah (24) hauzwi licha ya vilabu mbalimbali vya Ligi Kuu England kumtolea macho.
Arteta amebainisha kuwa nyota huyo raia wa England ni sehemu muhimu ya kikosi hicho kinachowania ubingwa wa Ligi Kuu England ambao hawajaupata kwa kipindi cha miongo miwili.
Licha ya nafasi finyu ya kuanza ndani ya kikosi cha Arsenal Nketiah ndio kinara wa magoli klabuni hapo kwenye Ligi Kuu England akiwa na magoli 5 sawa na Bukayo Saka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live