Wed, 27 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Washika mitutu wa London, Arsenal "The Gunners" wametinga hatua ya Robo Fainali baada ya kugaragaza Leeds United magoli 2-0.
Mabao ya Calum Chambers dakika ya 55 na Eddie Nketiah dakika ya 69 yameipa Arsenal ushindi wa 2-0 dhidi ya Leeds United usiku wa Jumanne Uwanja wa Emirates Jijini London na kutinga Robo Fainali ya Kombe la Ligi England.
Michezo mingine itaendelea usiku wa Leo ili kujua timu nyingine zitakazoingia hatua hiyo ya Robo Fainali.
Preston North End watawakaribisha Liverpool, West Ham vs Man City.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live