Fri, 11 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Arsenal Usiku wa Jana walihitimisha safari ya michezo mitano pasipo kupata matokeo ya ushindi baada ya kuichapa Wolves bao 1-0.
Bao pekee la Gabriel Martinelli dakika ya 25, limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 dhidi ya Wolverhampton Wanderers usiku wa Alhamisi Uwanja wa Molineux, Wolverhampton, West Midlands.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 39 katika mchezo wa 22 na kupanda nafasi ya tano ikiizidi wastani wa mabao Manchester United, ambayo pia imecheza mechi moja zaidi.
Wolves inabaki na pointi zake 34 za mechi 22 katika nafasi ya nane.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live