Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Arsenal waishushia kipigo kizito West Ham

IMG 8814.jpeg Arsenal waishushia kipigo kizito West Ham

Mon, 12 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Timu ya Arsenal imeibuka na ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya West Ham United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Jumapili Uwanja wa London Jijini London.

Mabao ya Arsenal yamefungwa na William Saliba dakika ya 32, Bukayo Saka mawili dakika ya 41 kwa penalti na dakika ya 63, Gabriel Maghaelhas dakika ya 44, Leandro Trossard dakika ya 45 na Declan Rice dakika ya 65.

Kwa ushindi Arsenal inafikisha pointi 52 katika mchezo wa 24, ingawa inabaki nafasi ya tatu ikizidiwa wastani wa mabao na Manchester City ambao pia wana mchezo mmoja mkononi.

Kwa upande wao West Ham United baada ya kichapo hicho wanabaki na pointi zao 36 za mechi 24 nafasi ya nane.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live