Ligi Kuu England inaendelea tena leo Oktoba 8, 2023 kwa mechi nne lakini kubwa kuliko ni mpambano kati ya Mabingwa Watetezi dhidi ya Washindi wa Ngao ya Jamii 2023, katika dimba la Emirates.
Liverpool ambao wamekuwa na msimu bora mpaka sasa wataendelea kuzisaka alama tatu wakiwa wageni wa Brighton katika dimba la AMEX majira ya saa 10, 2023.
Arsenal vs Man City
Uwanja: Emirates
Muda saa 18:30 jioni
Mwamuzi: Michael Oliver
Brighton vs Liverpool
Uwanja : AMEX
Muda : saa 10:00 jioni
Mwamuzi: Anthony Taylor
16:00 West Ham United vs Newcastle
16:00 Wolves vs Aston Villa
Kuelekea mchezo Arsenal huenda ikamkosa winga Bukayo Saka kutokana na majeraha huku mlinzi Jurrien Timber akiendelea kuwa nje kwa majeraha.
Kwa upande wake Man City itaendelea kumkosa Kevin de Bruyne kwa majeraha huku kiungo Rodrigo akikosa mchezo huu kutokana na adhabu ya kadi nyekundu aliyopata dhidi ya Nottingham Forest.