Klabu ya Arsenal itashuka dimbani leo kuwakaribisha klabu ya Manchester City katika dimba lao la Emirates katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza katika vita ya kuwania ubingwa wa ligi kuu ya England.
Klabu ya Arsenal ambayo imetoka kudondosha alama katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza itakwenda kukutana na Manchester City ambayo imetoka kushinda mchezo wa ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Aston Villa, hivyo mchezo wa leo utakua wenye ushindani mkubwa kutokana na ubora ambao upo ndani ya vilabu hivyo.
Klabu ya Manchester City chini ya kocha Pep Guardiola imekua haipo kwenye ubora ambao umezoeleka kwa miaka kadhaa, Lakini katika mchezo wa leo dhidi ya washika bunduki wa London inaonekana kama mchezo muhimu zaidi kwa Man City kwani wakishinda mchezo wa leo watapata nafasi ya kwenda kileleni.
Klabu ya Arsenal chini ya kocha Mikel Arteta wamekua kwenye ubora mkubwa msimu huu licha ya kutopata matokeo katika michezo mitatu mfululizo mpaka sasa, Lakini mchezo wa leo utakua na umuhimu kwa klabu hiyo na kutaka kurudi kwenye njia ya ushindi.
Vita nyingine katika mchezo huu ni baina ya makocha wawili ambapo Pep Guardiola atakutana na mwanafunzi wake Mikel Arteta ambae amekua kwenye ubora mkubwa siku za karibuni, Mchezo wa leo utakua chachu ya zile mbio za ubingwa msimu huu kwa yeyote atakaeshinda mchezo huo.