Thu, 23 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa wa Ulaya, Chelsea wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Carabao Cup baada ya ushindi wa 2-0 dhidi Brentford usiku huu Uwanja wa Brentford Community mjini Brentford, Middlesex.
Mabao ya Chelsea yamefungwa na Pontus Jansson aliyejifunga dakika ya 80 na Jorginho kwa penalti dakika ya 85 na kwa ushindi huo The Blues ya kocha Thomas Tuchel itakutana na Tottenham Nusu Fainali.
Mchezo mwingine wa nusu Fainali utakua ni Arsenali dhidi ya Liverpool, na michezo hiyo ya mzunguko wa kwanza itapigwa Januari 2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live