Mamlaka nchini Argentina imesitisha sherehe za kufurahia ubingwa wa Kombe la Dunia zilizokuwa zikiendelea nchini humo kutokana na mamilioni ya watu kusongamana katika mji wa Buenos Aires hali iliyopelekea kifo cha shabiki mmoja pamoja na majeruhi.
Mamlaka nchini Argentina imesitisha sherehe za kufurahia ubingwa wa Kombe la Dunia zilizokuwa zikiendelea nchini humo kutokana na mamilioni ya watu kusongamana katika mji wa Buenos Aires hali iliyopelekea kifo cha shabiki mmoja pamoja na majeruhi. Pia vilevile shirikisho la soka nchini humo lilisitisha msafara wa basi la wachezaji na kuwarudisha majumbani kwao baada ya mashabiki wawili kujirusha kutokea juu ya daraja mpaka kwenye basi la wachezaji.