Thu, 15 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF limemteua mwamuzi wa Tanzania, Ahamed Ally Arajiga kutokea mkoani Manyara kusimamia mchezo wa Klabu Bingwa Africa CAF kati ya Red Star kutoka Afrika ya Kati na Djoliba AC de Bamako kutoka Mali.
Mchezo huo utachezwa Jumamosi, Agosti 17 saa 17:00 jioni katika Uwanja sa Stade Japoma nchini Mali.
Arajiga ndiye mwamuzi bora wa kati kwa sasa nchini Tanzania akiwa amenyakua tuzo hiyo kwa misimu miwili mfululizo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live