Wed, 5 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aprili 2023, huenda ndio mwezi mgumu zaidi kwa Kariakoo Brothers (Simba Sc na Yanga Sc).
Aprili kuna robo fainali michuano ya CAF ambapo wote wapo, kwa kupenda kwao kushindana ikitokea mmoja ametoka na mmoja amepita itakuwa nongwa.
Aprili hii hii kuna Derby ya Kariakoo, ikitokea mmoja kapigwa tena awe yule yule ambaye hajapita kwenye CAF basi hapatakalika.
Ikitokea ambaye hajapita CAF kaja kushinda Derby basi hapo kidogo patazungumzika, ni Aprili ngumu sana kwa Kariakoo Brothers.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: