Klabu ya Aswan inayoshiriki Ligi daraja la pili nchini Misri imefungiwa na FIFA kufanya usajili kwa miaka mitatu kutokana na kutenda kosa la kumlazimisha aliyekuwa nyota wao Raphael Ayagwa raia wa Nigeria kusaini mkataba kwa Lugha asiyoielewa (Kiarabu).
Klabu ya Aswan inayoshiriki Ligi daraja la pili nchini Misri imefungiwa na FIFA kufanya usajili kwa miaka mitatu kutokana na kutenda kosa la kumlazimisha aliyekuwa nyota wao Raphael Ayagwa raia wa Nigeria kusaini mkataba kwa Lugha asiyoielewa (Kiarabu). Wakala wa nyota huyo amesema maofisa wa Klabu hiyo walimfungia yeye nje wakati nyota huyo anaenda kusaini lakini baadae wakaanza kumlazimisha huku wakimtamkia maneno ya kutisha ili aogope asaini mkataba huo ambao ulikuwa umeandikwa kwa Lugha ya kiarabu.