Kocha Carlo Ancelotti ameendelea kushikilia rekodi yake ya kutopoteza mchezo dhidi ya waajiri wake wa zamani Bayern Munich, baada ya ushindi wa mabao mawili kwa moja uliompeleka hatua ya fainali ya Ligi ya Mabingwa barani ulaya.
Kocha Carlo Ancelotti ameendelea kushikilia rekodi yake ya kutopoteza mchezo dhidi ya waajiri wake wa zamani Bayern Munich, baada ya ushindi wa mabao mawili kwa moja uliompeleka hatua ya fainali ya Ligi ya Mabingwa barani ulaya. Rekodi nyingine kwa Carlo Ancelotti, endapo ataingoza klabu yake Real Madrid kushinda taji la UEFA Champions League msimu huu 2023-2024, atakuwa ameweka historia ya kuwa Kocha wa kwanza kushinda Makombe Matano ya Ligi ya Mabingwa barani ulaya.