Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti ndie Kocha anaepewa kipaumbele katika nafasi ya kukinoa kikosi cha Timu ya Taifa ya Brazil.
Kocha huyo mwenye mafanikio makubwa kwa ngazi ya Vilabu, hana msimu mzuri akiwa na Real Madrid msimu huu huku taarifa zikidai kuwa atatimuliwa.
Akizungumza Rais wa Chama cha Soka Brazil anasema;
“Ninampenda sana Ancelotti. Yeye sio kipenzi cha wachezaji tu bali pia mashabiki. Popote ninapoenda Brazil, Ancelotti ndilo jina la kwanza ambalo wafuasi wananiuliza kuhusu”
Brazil inahaha kusaka Kocha baada ya kumtimua Tite huku kikipita kipindi kirefu pasipo kufanya vyema.