Wakati huu ambapo Kiungo wa Real Madrid na Croatia, Luka Modric anahisishwa na vilabu mbalimbali, Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti amejibu kuhusiana taarifa hizo.
Luka Modrić hataondoka Real Madrid Januari", anasema Carlo Ancelotti
“Hakuna nafasi kwa Luka kuondoka Januari. Hataki kuondoka na tunafurahi sana kuhusu hilo”.
"Anafikiri yeye ni mchezaji muhimu na tunafikiri vivyo hivyo - kwa kuwa ni mchezaji muhimu sana kwetu".
“Modrić hafurahii muda wa mchezo na hiyo ni dhahiri lakini mimi huzungumza naye kila siku… bado ana ari zaidi”.
“Hakuna mtu kama yeye ndani ya chumba cha kubadilishia nguo… yeye ndiye kiongozi. Umuhimu wake ni mkubwa kwa Real Madrid”.
“Nampenda sana, sote tunampenda Luka”.