Cairo, Misri. Kocha Emmanuel Amuneke ametimuliwa kuwa kocha wa Misr El-Makkasa ya Misri mwezi moja tangu alipopewa jukumu hilo sasa atakuwa mkurungezi wa akademi za klabu hiyo itakayofungua kituo cha kwanza hivi karibuni Tanzania.
El-Makkasa ilitangaza kumpa kazi ya ukocha Amuneke mwezi Februari 2 baada ya kuachana na kocha Ahmed Hossam Mido.
Klabu hiyo ilitoa taarifa yake jana Jumapili, kuwa kumtaja Ehab Galal kuwa kocha mpya anayechukua jukumu la Amuneke aliyepangiwa kazi nyingine.
"Tumefikia makubaliano na Ehab Galal kuiongoza timu kuanzia katika mchezo wa leo Jumatatu dhidi ya Aswan katika Ligi Kuu Misri," ilisema taarifa hiyo.
"Amuneke atakuwa mkurungezi wa akademi za klabu ambazo tumepanga kuzifungua katika sehemu mbalimbali barani Afrika, kituo cha kwanza kitafunguliwa hivi karibuni Tanzania", iliongeza taarifa ya El-Makkasa.
Amuneke aliiongoza El-Makkasa katika michezo mitatu tu dhidi ya Smouha na Al Entag Al Harbi akipata sare mbili za bao 1-1, kabla ya kufungwa 1-0 na Tala'ea El Gaish katika Kombe la Misri.
Pia Soma
- Manara atoa vifaa vya michezo Arumeru
- Solskjaer amkingia kifua De Gea
- Samatta amchongea beki wa Manchester City