Mon, 8 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars Adel Amrouche amesema amefurahishwa na kiwango cha baadhi ya nyota aliowaita kwenye kikosi chake akiwemo Mohamed Hussein 'Tshabalala'.
Kocha huyo ameyasema hayo mara baada ya kukamilika kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Misri ambayo ilimalizika kwa Stars kufungwa 2-0.
"Nimefurahishwa na viwango vya baadhi ya wachezaji, nimependa ujio mpya wa Tshabalala na wachezaji wengine," alisema Amrouche.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live