Fri, 5 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki wa Azam FC, Daniel Amoah, ameongeza mkataba wa miaka miwili zaidi kuendelea kusalia ndani ya viunga vya Azam Complex.
Amoah amesaini mkataba huo mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat', utakaomalizika Agosti 2024.
Haikuwekwa wazi mkataba wake wa awali na timu hiyo, ulikua unatarajia kumalizika wakati gani.
Azam kwa sasa inajiimarisha ili kuwabakisha nyota wake ikiwa ni mipango ya kuhakikisha wanafanya vyema ligi Kuu ya NBC 2021/2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live