Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ambokile arejeshwa Mbeya City, Haule bado kidogo tu

Eliud Ambkokile Straika Mpya wa Mbeya City, Eliud Ambokile

Sat, 14 Aug 2021 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

Mbeya. Wakati joto la usajili likizidi kupamba moto kwa timu mbalimbali hapa nchini, Mbeya City inatajwa kumalizana na nyota wanne, huku ikiwa hatua za mwisho kumnasa Kipa wa Azam, Benedict Haule kwa mkopo.

Timu hiyo ya jijini hapa katika msimu uliopita licha ya kumaliza nafasi ya 10, lakini haikuwa na mwanzo mzuri hadi kusubiri mechi mbili za mwisho na kujihakikishia kukusanya alama 42.

Taarifa ilizopata Mwanaspoti kutoka ndani ya klabu hiyo ni kuwa tayari imekamilisha usajili wa nyota wapya wanne akiwamo aliyekuwa Straika na mfungaji wake wa muda wote, Eliud Ambokile.

Wengine waliosaini hadi sasa ni Straika wake wa zamani, Paul Nonga kutoka Gwambina, Pato Ngonyani (Polisi Tanzania) na Frank Ikibela aliyerejeshwa tena kikosini kutoka Ruvu Shooting.

Hata hivyo inadaiwa kuwa timu hiyo inatarajia kutangaza usajili wake kuanzia wiki ijayo pamoja maandalizi ya jumla ya msimu ujao ikiwamo kambi ambayo inatazamiwa kuanza Agosti 26 mwaka huu.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz