Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Amadou Haidara atakuwa usajili wa kwanza wa Ralf Rangnick?

Amadou Haidara Amadou Haidara

Sun, 5 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo wa RB Leipzig Amadou Haidara anatajwa kuwa atakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Manchester United chini ya meneja mpya Ralf Rangnick.

Mashetani Wekundu watakuwa chini ya ulezi wa muda wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 63 kwa mara ya kwanza Jumapili hii kwenye gemu ya Ligi Kuu dhidi ya Crystal Palace.

Rangnick amekiri kwamba uhamisho wa Januari utakuwa mgumu kwa klabu, lakini Haidara anafikiriwa kuwa mmoja wa wachezaji wanaolengwa zaidi na Mjerumani huyo kwenye dirisha la uhamisho la majira ya baridi.

The Sun wameripoti kwamba United wanajiandaa kutumia kipengele chake cha kuachiliwa cha pauni milioni 32 mwezi ujao huku Rangnick akikaribia kusajili mchezaji wake wa kwanza wa Red Devils.

Ripoti hiyo inaongeza kuwa Rangnick amekubali dili la mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kufuatia mazungumzo na wakala wake, na ushiriki wake katika Kombe la Mataifa ya Afrika na Mali hautaleta changamoto.

Haidara anajivunia mabao 10 na asisti sita katika mechi 100 akiwa na Leipzig katika mashindano yote, na mkataba wake na timu hiyo ya Bundesliga unaisha mwaka 2025.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live