Thu, 27 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Taarifa zinadai kuwa kesho kutakuwa na sapraizi kwenye lango la Simba katika mchezo dhidi ya Wydad nchini Morocco.
Kipa mzoefu ambaye hajadaka siku nyingi, Beno Kakolanya ataanza akichukua nafasi ya Ally Salim ambaye ameonyesha umahiri mkubwa kwenye siku za karibuni.
Kakolanya hakucheza mchezo wowote tangu kukosekana kwa Aishi Manula huku taarifa zisizo na uhakika zikidai yuko mbioni kuondoka Klabuni hapo kujiunga na Singida Big Stars.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live