Tue, 15 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Afisa Habari wa Yanga African, Ally Kamwe amesema wanafahamu kuwa watapata idadi ndogo ya mashabiki katika mchezo wao wa Jumapili Agosti 20,2023 pale Azam Complex lakini ipo pia faida ya uwanja huo.
Yanga wanatarajia kuanza hatua ya awali ya mchezo wa klabu Bingwa dhidi ya Asas ambapo michezo yote miwili itapigwa kwenye uwanja huo.
"Tutacheza Chamazi tunafahamu itakuwa ni idadi ndogo ya mashabiki lakini faida ni kwamba pale itakuwa ni full house na uwanja upo karibu na mashabiki hivyo itakuwa rahisi kutoa hamasa kwa wachezaji wetu," alisema Ally Kamwe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live