Wakati Stori zikizidi kusambaa kuwa Mshambuliaji wa Yanga Fiston Klala Mayele yuko mbioni kutimka ndani ya Klabu hiyo huku akihusishwa na Klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika ya Kusini.
Msemaji wa Yanga Ally Kamwe ametoa kauli yake kuhusiana na taarifa ya mchezaji huyo.
Akizungumza kupitia Clouds FM Kamwe anasema;
“Tulitegemea kupokea ofa Barani Afrika na nje ya Bara la Afrika ,ni kweli tumepokea ofa kutoka Klabu nyingi lakini tumeseti mipango yetu”
“Hatupo tayari kupoteza Wachezaji wetu bora ikishindikana atazungumza na Klabu, hii ni Klabu inayotoa fursa ukija ukiagana vizuri na Viongozi unapewa baraka unaondoka"