Mon, 23 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji Emmanuel Mahop Dikongue (28) aliyekuwa akihusishwa kujiunga na Yanga kwenye dirisha lililopita la usajili atajiunga na Coton Sport ya nchini Cameroon.
Mahop alifunga mabao kumi na nne (14) kwenye Ligi kuu ya Cameroon msimu uliopita akiwa Canon Yaoundé, Emmanuel Mahop atasaini mkataba wa mwaka mmoja akiwa Mchezaji huru.
Mahop atasaini Coton Sport akiwa Mchezaji huru (Free agent) baada ya kutoka nchini Saudi Arabia ambapo alifeli majaribio katika Klabu inayoshiriki Ligi daraja la kwanza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live