Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyembusu mwanasoka wa kike aendelea kukaliwa kooni

Aliyembusu Mwanasoka Wa Kike Aendelea Kukaliwa Kooni Aliyembusu mwanasoka wa kike aendelea kukaliwa kooni

Thu, 28 Mar 2024 Chanzo: Bbc

Waendesha mashtaka wa Uhispania wanataka aliyekuwa mkuu wa shirikisho la soka nchini humo afungwe jela miaka miwili na nusu, baada ya kumbusu mwanasoka wa kike dhidi ya hiari yake katika ushindi wa Kombe la Dunia wa Uhispania.

Luis Rubiales anakabiliwa na mashtaka ya unyanyasaji wa kijinsia na kutumia nguvu baada ya kumshika Jenni Hermoso na kumbusu mdomoni Agosti mwaka jana.

Bi Hermoso na wachezaji wenzake walisema busu hilo halikutakikana na lilidhalilisha.

Bw Rubiales alilazimika kujiuzulu, lakini amekanusha makosa yoyote.

Kulingana na hati ya mahakama iliyoonekana na Reuters, mwendesha mashtaka Marta Durantez alimshtaki Bw Rubiales kwa shtaka moja la unyanyasaji wa kijinsia na moja la kulazimishwa kwa madai yake ya vitendo baada ya busu. Mashtaka hayo yana vifungo vya mwaka mmoja na miezi 18 mtawalia.

Bi Durantez pia alimshutumu kocha wa zamani wa timu ya taifa ya wanawake, Jorge Vilda, mkurugenzi wa sasa wa michezo wa timu hiyo, Albert Luque, na mkuu wa soko wa shirikisho hilo, Ruben Rivera, kwa kumlazimisha Bi Hermoso kusema busu hilo lilikuwa la maelewano.

Shtaka lilisema walimnyanyasa kupitia "vitendo vya mara kwa mara vya kumpa shinikizo", ikiwa ni pamoja na kupitia marafiki na familia yake.

Wote watatu walikanusha kutanda makosa hayo walipofika mbele ya mahakama. Kila mmoja anaweza kufungwa jela miezi 18 iwapo atapatikana na hatia.

Bi Durantez pia anataka wanaume hao wanne walipe fidia ya jumla ya €100,000 (£85,677; $108,000) kwa Bi Hermoso, na Bw Rubiales alipe angalau nusu ya kiasi hicho.

Pia aliomba amri ya kuzuiwa kwa Bw Rubiales, ikimzuia kufika umbali wa mita 200 (futi 656) kutoka kwa Bi Hermoso na kuwasiliana naye kwa miaka saba na nusu ijayo.

Kashfa hiyo ilikuwa gumzo wakati wa kihistoria kwa timu ya wanawake ya Uhispania, ambayo wakati huo ilikuwa ikisherehekea ushindi wake wa kwanza wa Kombe la Dunia.

Wakati wa hafla ya kukabidhi kombe, Bw Rubiales alikishika kichwa cha Bi Hermoso katikati ya mikono yake na kumpiga busu kwenye midomo yake.

Chanzo: Bbc