Wed, 31 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Sharaf Eldin Shaiboub Ali aliyekuwa mchezaji wa klabu ya APR FC ya Rwanda ametambulishwa katika timu ya Al Hilal SC Benghazi ya Libya kama mchezaji mpya.
Mchezaji huyo raia wa Sudan inasemekana kuwa amewalipa APR FC Dola Elfu 70 ili aweze kuondoka katika timu hiyo ambao ni Wawakilishi wa Rwanda Ligi ya Mabingwa Afrika.
Sharif Eldin Shaiboub aliwahi kukipiga katika klabu ya Simba SC kabla ya kutimkia APR FC ya Rwanda.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live