Sat, 23 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa Kiungo wa ushambuliaji wa klabu ya Al Hilal Omdurman ya Sudan, Lamine Jarjou (21) amejiunga na klabu ya Grenoble Foot 38 inayoshiriki Ligi daraja la pili nchini Ufaransa.
Jarjou amesaini mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo na atavaa jezi namba 12.
Dirisha kubwa la Usajili, Lamine Jarjou alihusishwa kutua ndani ya klabu ya Azam ila makubaliano baina ya klabu na klabu hayakufikiwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live