Wed, 23 Dec 2020
Chanzo: millardayo.com
Mshambuliaji wa FC Lupopo ya DR Congo, Mpiana Mozinzi, amejiunga na Klabu ya Azam ya jijini Dar es Salaam, akitarajia kuasaini mkataba wa mwaka mmoja kesho.
Mozinzi alihusishwa kutua Yanga na Simba katika kipindi cha dirisha kubwa msimu huu, lakini dili hizo hazikufanikiwa.
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Azam FC, Zakaria Thabiti, amesema mchezaji huyo amewasili nchini leo mchana na atafanyiwa vipimo vya afya, akifanikiwa ataanza kuitumikia rasmi timu hiyo.
ZIMBABWE PAGUMU SIMBA SC WAJIPANGE “KUCHEZA BILA MASHABIKI HASARA KWA SIMBA SIO MWENYEJI PLATNUM”
Chanzo: millardayo.com