Dar es Salaan. Beki wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Banda amesema hana maambukizi ya virusi vya corona.
Banda anayecheza Highlands Park ya Afrika Kusini hana virusi hivyo ambavyo vimeleta taharuki duniani.
Awali, Banda alionekana na dalili ya ugonjwa huo, lakini majibu ya jana yamethibitisha yuko vizuri kiafya.
“Nilikuwa nikijihisi hivyo nikachukua hatua ya kufanyiwa vipimo, jambo jema majibu yametoka nipo salama,” alisema Banda.
Muda mfupi baada ya majibu alishukuru Watanzania waliokuwa pamoja naye katika kipindi alichokuwa akihisi ugonjwa huo.
Banda aliwataka Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya virusi hivyo vilivyotikisa dunia.
Habari zinazohusiana na hii
- Hali ya Abdi Banda baada ya kuchukuliwa vipimo vya Corona
- Majibu ya Abdi Banda baada ya kupima Corona