Thu, 2 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Tambo za Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe zimejiri baada ya timu hiyo kutinga nusu fainali ya Kombe la Shirikisho (FA) kwa kuichapa Tabora United kwa mabao 3-0, mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi Mei 01, 2024.
Kamwe amesema, Yanga imepokea ofa kutoka Urusi, Israel ambapo kuna timu zinamtaka Clement Mzize, huku akisisitiza mshambuliaji mwingine, Joseph Guede ni mchanganyiko wa Didier Drogba, Fernando Torres na Thierry Henry.
Msemaji huyo akauliza 'Je mme 'enjoy' kumuona Pacome akicheza kwa kutumia mguu mmoja?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live