Wakati wadau na wachambuzi mbalimbali wa Soka wakisifu ubora wa Yanga waliouonesha katika mchezo wa Dabi ya Karikoo jana Novemba 5 na kuibuka na ushindi wa mabao 5-1.
Mchambuzi wa Michezo kutoka TV3 Alex Ngereza amesema kuwa sio kweli kwamba Yanga walikuwa Bora kuliko Simba katika mchezo huo.
Ngereza anasema;
"Guys sio kwamba Yanga walikuwa bora sana kuliko Simba ila Simba wamefanya makosa mengi kwenye maeneo hatari na kama Simba wangecheza kama ambavyo walicheza dhidi ya Al ahly hapa Nyumbani na kule ugenini Simba wasingefungwa magoli mengi kiasi hiki
Angali magoli mfano goli la nne Max Nzegeli amekutwa na mpira akiwa peke yake kabisa na ukiacha goli hilo angalia tena goli penalty Inonga ameenda kufanya tackling vibaya akamgusa mtu badala ya kugusa mpira
Makosa kama haya ambayo Simba wamefanya leo dhidi ya Yanga ilikuwa lazima waadhibiwe Kutokana na ubora wa wachezaji waliopo kwenye kikosi cha yanga"