Kocha Mkuu wa Yanga SC, Miguel Gamondi, amesema kesho wana kila sababu ya kushinda dhidi ya Medeama.
"Ni lazima tushinde mechi yetu ya kesho mbele ya Medeama ili tufuzu hatua inayofuata, najua sio rahisi ila tutaweza kesho kupata alama, tumepata alama moja kwenye kundi ila timu yetu imefanya vizuri kwenye michezo iliyopita”
“Leo ndio nitajua kwenye maandalizi yetu ya mwisho nini nitaenda kufanya ila alama tatu za kesho ni lazima kwa sababu ni muhimu kwetu."
Yanga kesho wanacheza mchezo huo muhimu ugenini wa hatua ya Makundi ya Klabu Bingwa Afrika baada ya kufungwa 3-0 na CR Belouizdad na kutoka sare ya 1-1 na Al Ahly.