Sun, 15 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Al Nassr ya Saudia Arabia, Rudi Garcia amekutana na Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid, Eden Hazard ofisini kwake nchini humo.
Al-Nassr ambayo hivi karibuni ilimsajili Cristiano Ronaldo, sasa inataka kumsajili Eden Hazard, Kocha Rudi Garcia ambaye anamfahamu Hazard toka akiwa katika klabu ya Lille, mazungumzo hayo ni sehemu ya kumshawishi ajiunge msimu huu wa joto.
Utakumbuka, Hazard ameripotiwa kugoma kuondoka Real Madrid na kudai atabaki klabuni hapo kugombea namba kwenye kikosi cha Carlo Ancelotti hadi mwisho wa mkataba wake 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live