Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Al-Merrikh kutua nchini kesho

Yanga Vs Merrikh 2 0.jpeg Al-Merrikh kutua nchini kesho

Tue, 26 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wapinzani wa Yanga katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Merrikh ya Sudan, wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam, kesho Jumatano.

Msafara wa kikosi hicho unatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar majira ya 9:00 Alasiri, ukitokea Rwanda kwa Shirika la Ndege la RwandAir.

Ofisa Habari wa Yanga SC, Ally Kamwe, amebainisha kwamba: “Wenzetu Al Merrikh wataingia kesho majira ya saa tisa kamili alasiri, kwa Shirika la Ndege ya Rwanda.

“Tumesikia kauli za Kocha wa Al Merrikh anasema kuwa Yanga SC inaogopeka Afrika. Sisi tumesoma Cuba, tunamwelewa, hawezi kutuchota, tutauchukulia mchezo kwa umakini mkubwa.

“Kocha wa Al Merrikh amesema pia anakuja kufunguka hapa, kwetu sisi ni taarifa njema kwa sababu mnara haukusoma Rwanda, hivyo tukipishana nao itakuwa fursa ya kusimamisha mnara.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: