Mon, 19 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Al-Hilal imeripotiwa kufikia makubaliano binafsi na beki kisiki wa Chelsea, Kalidou Koulibaly, 31, na kwa sasa inapambana kuishawishi Chelsea ikubali kuwauzia.
Koulibaly ambaye hajafanya vizuri sana kwa msimu uliopita anadaiwa kupewa ofa maradufu ya mshahara ambao anaupata kwa sasa Chelsea.
Mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwaka 2026. Msimu uliopita alicheza mechi 33 za michuano yote.
Tayari Al Hilal wameshakamilisha usajiliwa Kiungo wa Kireno Ruben Neves kutoka Wolves.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live