Wed, 26 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Al Ahly imezawadiwa ushindi wa alama tatu mabao 2-0 dhidi ya Zamalek baada ya timu hiyo kukataa kucheza derby ya Cairo, jana Jumanne, Juni 25, 2024 katika mchezo ulioahirishwa wa msimu wa 2023/24 wa Ligi Kuu ya Misri.
Zamalek walikataa kucheza mechi hiyo kwa sababu matakwa yao ya hapo awali kuhusu uendeshaji wa Ligi Kuu ya Misri hayakutimizwa huku wakidai kuwa hawachezi mechi yoyote mpaka Al Ahly na timu nyingine zimalize viporo vyao (mechi zilizoahirishwa).
Kariakoo derby achezeshe mwamuzi wa hapa nchini au atokee nje?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live